Roberto Di Matteo
Anton Ferdinand na John Terry
Anton Ferdinand
"Tunajiamini ," alisema Di Matteo kuhusu mechi yao na Arsenal mchana wa leo. "hivyo hatujali sana kitu gani watu huko nje hunena juu yetu. Ni lazima tujiangalie nguvu yetu juu ya mchezo na huo ndiyo mwenendo wetu."
"Hivyo ndivyo nionavyo na nihisivyo. Siwezi kuwaza eti watu wengine wana maoni gani. Tunachoweza kufanya ni kuwaza ni namna gani tunacheza na tunavyojiheshimu na kujitunza. Lazima tujiweke kwenye hali nzuri. Na hata mwisho wa siku tunajua kwa hakika wapenzi wa timu pinzani hawatatupenda."
"Hayo ndiyo maneno yangu kwa ujula. Hivyo hatutapoteza nguvu nyingi kuwa na wasi wasi juu ya nini wanawaza. Ni lazima tujifikirie wenyewe, tujaribu na kushinda mechi kwa timu yetu."
Terry atakuwepo kwenye mechi ya leo, pamoja na kukosa siku kadhaa za mazoezi ili ahudhurie kesi yake huko Wembley.
Di Matteo alisema kwamba kila kitu kitaendelea kama kawaida na kwamba atachagua timu yake kwa mujibu wa Emirates pekee.
"Uchgauzi wangu mimi ni wa kawaida tu." Alisema Di Matteo. "Ninavyoweza kuona Terry yupo fit. kutakuwa na taratibu za kawaida tu. Itakuwa ni kazi yangu kuchagua timu itakayoipiga Arsenal."
Terry ana uwezo wa kucheza vizuri tu bila kujali mambo ambayo inaonekana yatawachanganya wengine, na Di Matteo anaona hakuna chochote cha kupoteza leo.
Wakati bosi wa Chelsea alieleweka kuchukua tahadhari kuzungumzia ishu za hivi karibuni, alimsifu kwa hasaka Terry na tabia yake kwa upande wa kazi awapo uwanjani. "Niwezayo kusema ni kazi yake awapo kwenye timu." Alisema Di Matteo.
"Siku zote yeye ni wa kwamba kuwasili. Ana jitihada sana na amekuwa ni mtumishi mzuri sana wa timu yake.
Chelsea walianza Premier League vizuri na wapo kileleni, lakini Arsenal watakuwa ni wapinzani wao hatari sana kwa msimu huu.
"Utakuwa ni mtihani mgumu, alikubali Di Matteo. "Arsenal siku zote ni mtihani mgumu, ni changamoto kubwa kwetu. Lakini na kwao pia itakuwa ni changamoto kubwa, kwani sisi ni timu ngumu na nzuri pia.
Ingawaje Arsenal walimuuza Robin van Persie na Alex Song, Di Matteo alisema alitabiri kwamba wangekuwa ni tishio kwao tangu mwanzo.
"Nilisema mwanzoni mwa msimu kwamba Arsenal wataleta changamoto kwenye ligi," alisema meneja huyo. "Sina uhakika kama kuna aliyeniamini, lakini hivyo ndivyo nilivyooona mimi, na sijabadili mawazo yangu."
"Sidhani kama wana namna nyingine tofauti ya kucheza. Wanacheza kwa kumiliki sana mpira na kuutafuta wanapoupoteza, lakini Lukas Podolski na Gervinho wamekuwa wakifunga magoli, na Santi Cazorla. Wanao wachezaji ambao ni tishio na wenye uwezo wa kubadilisha nafasi." Alisema Di Matteo.
Kama wewe ni mshabiki wa Arsenal au Chelsea, unasemaje kuhusu mechi ya leo?
0 comments:
Post a Comment