Didier Drogba amesisitiza kwamba anayafurahia sana maisha ya Uchina na kwamba anategemea kukamilisha mkataba wake wa miaka miwili na nusu wa kuchezea soka lake kwenye timu yake mpya ya Shanghai Shenhua.
Lakini Drgba mwenye amesema kwamba anatarajia kubakia China hadi mwisho wa mkataba wake na hata zaidi ya hapo.
Drogba ameshafunga magoli matano kwenye mechi saba hadi sasa kwenye Chinese Super League.
"Nimewasili kama miezi miwili tu iliyopita, hivyo nina furaha sana. Nina furahia sana hapa hivyo sina sababu ya kuondoka. Sitaki kuondoka hapa."
Drogba alifunga magoli 157 ndani ya miaka nane aliyochezea Chelsea na kufanikiwa kuchukua Champions League kwa mara ya kwanza msimu uliopita.
"Nataka kubakia hapa, ili mradi tu niendelee kushinda mataji mbali mbali kwa timu yangu na kuwafurahisha maashabiki wetu." Aliongezea Drogba.
"Ni ngumu sana kwa sasa lakini natumaini kuna matumaini na ndivyo ninavyoamini."
Drogba, ambaye alikanausha taarifa za kwamba alikuwa halipwi na klabu yake, alielezea kushinda kwa champions League akiwa na Chelsea, akifunga goli la ushindi kwa penati kama "the best moment of my career."
"kuwa na uwezo wa kushinda mechi kama ile ni kitu kizuri kisichosahaulika kamwe." Alisema.
"Lakini ni lazima uendelee na maisha, hivyo kwa sasa nazingatia yale ninayoweza kuyafanya kwa ajili ya Chinese League. Natumaini ndani ya miaka michache, wakati mkataba wangu unaisha, nitakaa nanyi na kuongelea jinsi ilivyo nzuri kushinda Asian Champions League."
0 comments:
Post a Comment