Ni miaka saba sasa tangu Arsenal ichukue kombe, lakini sote tunafahamu hilo, na wana Arsenal wamechoka kusikia hiyo habari, ni wakati wa kuweka mambo sawa sasa.
Bodi inafahamu, meneja anafahamu, pia hata wewe unaweza kuhisi kuwa na wachezaji wanafahamu hilo.
Timu imefanya biashara nzuri kipindi hiki cha summer, mapema sana iliwasajili Podolski na Giroud ambao wote wawili watatazamiwa kufunga magoli msimu ujao.
Van Persie aliwaeleza ukweli mwezi Julai kwamba timu haina tamaa ya mafanikio-lakini kutia saini kwa Santi Gazorla kunaonesha kuwa timu ina mwelekeo mzuri.
Kumpoteza Alex Song itakuwa ni shida nyingine, lakini timu inajipanga kuziba pengo kwa kumtumia Yann M'vila. Mashabiki wangependa kusajiliwa kwa mshambuliaji mwingine machachari wa kuziba pengo la aliyekuwa kepteni wao Van Persie.
kuziba pengo la mshambuliaji aliyefunga magoli 30 kwenye premier league ni kazi ngumu sana. Na uwezo wa timu kiutendaji ndio utaonesha mafanikio na mapungufu yake.
Tunachouliza ni kwamba, "Je muda wa kutoatoa sababu umekwisha?" - Au umecheleweshwa tu kwa miezi 12.
Katika kipindi cha misimu michache iliyopita, moja ya sababu ambazo timu ilitoa za kushindwa kutwaa kombe ni kutokana na ma staa wake wengi kuuzwauzwa. Kwa huzuni, Van Persie ameendelea na utamaduni huo huo. Hapa swali ni kama Arsenal wamejipanga vya kutosha katika uhamisho wake ili kuziba mapengo yoyote.
Mashabiki wameshachoka na stori za timu. Arsenal wanaonekana kutatua matatizo kwa kuwasainisha mastaa wengine.
Hapa Wenger akiwa kazini. Picha na HTC Sport
Arsene Wenger ameleta maswali mengi sana juu ya mustakabali wake na Arsenal miezi 12 iliyopita. Lakini kwa vile alivyojipanga inadhaniwa mambo yatakuwa mazuri kwa upande wake msimu ujao hivi karibuni.
Wewe unasemaje? Kama Arsenal watamaliza tena bila kombe, je watakuwa na sababu zao zilezile?
0 comments:
Post a Comment