Mlinzi wa zamani wa Manchester United Denis Irwin amedai kwamba timu yake wataenda mbinguni na duniani katika harakati zao za kumtilisha saini kiungo wa Barcelona Cesc Fabregas msimu huu.
Arsenal wanaaminika kutaka kumsainisha tena nahodha wao huyo wa zamani kama yeye mwenyewe atapenda kuondoka Primera Division Champions na kurudi kwenye Premier League, lakini Irwin anapendekeza kuwa United wanashawishika kuwa na nafasi kubwa ya kumpata mwanandinga huyo mwenye umri wa miaka 26.
Irwin alikuwa ni miongoni mwa wasomi wa kwanza kudhihirisha United kumhitaji mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Robins Van Persie mwaka jana na sasa beki huyo wa zamani ambaye bado anafanya kazi kama balozi wa Old Trafford amedhihirisha kuwa Fabregas ndiyo tageti lao la mwisho.
"Cesc Fabregas ameongeza list ya wanaowaniwa na United na kupewa kipaumbele cha juu na mabingwa hao wataenda mbinguni na duniani ili kumnasa mkali huyo." Aliliambia gazeti kongwe la Sunday World.
"Mkali huyo wa Barcelona anataka kuondoka Nou Camp na United wanamuhitaji ile mbaya, hivyo dili itapaswa kufanywa kwa urahisi. Fabregas ni kiungo wa aina yake ambaye United wanahitaji iwapo wanataka kuendelea kutetea Ubingwa wao na Ligi ya mabingwa."
Irwin pia alitabiri kuwa United wanaonesha kumuhitaji Leighton Baines wa Everton na Luke Shaw wa Southampton, huku akipendekeza kuwa Winga machachari Nani na Beki mkongwe na mgumu kupitika Patrice Evra wataondoka Old Trafford msimu huu wakati meneja mpya David Moyes akijiandaa kuchukua mikoba ya Sir Alex Ferguson.
"Nani ataenda Monaco na Patrice Evra pia atarudi kwenye timu yake aliyokuwa kabla hajajiunga na United," alisema Irwin. "Nimesikia neno pia kwamba meneja mpya atamhitaji Luke Shaw kwenye list yake.
Monday, 10 June 2013
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment