Kikosi cha Stars
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars jana waliondoa matumaini ya kutinga Brazil kwa ajili ya fainali za kombe l dunia baada ya kukung'utwa magoli 4-2 katika mchezo mkali na wakuvutia uliochezwa jana kwenye uwanja wa Taifa Dar es salaam.
Mbwana Samata kulia, akiambaa na mpira
Stars waliokuwa wakishangiliwa kwa nguvu sana na umati wa mashabiki waliofurika uwanjani walipata bao katika dakika ya kwanza tu ya mchezo huo kupitia kwa mchezaji wao mahiri Amri Kiemba na kuwafanya Ivory Coast kuhaha sana na kufanikiwa kusawazisha goli hilo mnamo dakika ya 15 ya kipidi cha kwanza, na baadaye kuongeza bao la pili.
Ivory Coast wakishangilia goli
Katika dakika ya 38 Thomas Ulimwengu aliisawazishia Stars kwa kufunga bao la pili baada ya kupokea krosi mahiri toka kwa Shomari Kapombe. Na baadaye kabla ya kuisha kipindi cha kwanza Ivory Coast wakaandika bao la tatu kwa njia ya Penalty iliyopigwa na Yaya Toure anayekipiga MCFC. Hadi mapumziki Stars 2, Ivory Coast 3. Katika kipindi cha pili Ivory Coast wakaandika bao la nne na kuufanya mchezo uishe kwa 4-2.
Yaya Toure, pamoja na umaarufu wake lakini alikuwa anakabika tu
Timu ya Stars walionekana kulishambulia kwa nguvu sana lango la wapinzani wao lakini hali hiyo haikibadilisha matokeo yoyote kwani kosakosa ndizo zilizotawala.
Gervinho, naye alikabika vizuri tu
Ni kitu gani unadhani kuiimarishwe ama kiongezwe ili Stars iweze kucheza kombe la dunia au lili la mataifa ya Afrika?
Monday, 17 June 2013
Alimanusura Stars Wamuue Tembo!!! Ivory Coast Watinga Kumi Bora kwa 4-2
Posted on 00:36 by Unknown
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment