Sunday, 26 August 2012

Barclays English Premier League: Hivi Ndivyo Ilivyokuwa

Manchester City Dhidi Ya Liverpool
Hii ilikuwa ni Man City dhidi ya Liverpool. Ilikuwa ni moja ya mechi nzuri na kali sana tangu kuanza kwa English Premier League. 

Liverpool walionekana kujipanga vizuri zaidi na kuwapa shida sana walinzi pamoja na viungo wa Man City. 

Kama siyo makosa ya walinzi wa Liverpool ambao kwa namna moja au nyingine tunaweza kusema ndiyo waliochangia Man City kusawazisha magoli basi stori leo zingekuwa nyingine kabisa. 

Magoli ya Man City yalifungwa na Yahya Toure na Carlos Tevez na yale ya Liverpool yalifungwa na Martin Skrtel pamoja na Suarez

 Juu: Tevez alimpiga chenga kipa wa 
Liverpool na kusawazisha goli la pili 
kwa Man City baada ya mlinzi wa 
Liverpool Martin Skrtel kufanya 
makosa ya kurudisha mpira kwa 
goli kipa bila kuangalia kama kuna adui ama la.

 Juu: Hapa Tevez akishangilia baada ya 
kufunga goli la pili kwa timu yake




Juu:  Man City wakipongezana baada  
ya kusawazisha goli la kwanza
 kupitia Yahya Toure.

 Juu: Huyu ni kijana mdogo sana
 Raheem Sterling, Winga wa kushoto, 
mwenye umri wa miaka 17 tu. 
Alionesha kipaji cha hali ya juu na 
kusumbua sana walinzi wa Man City.





Arsenal Dhidi Ya Stoke City
Arsenal walishindwa kwa mara ya pili mfululizo kuwaridhishwa mashabi wao baada ya kutoka sare tena kwenye mchezo wao huo wa jana. 

 Hawa ni mashabiki wa Stoke City
 wakiwa na Mask za Arsene Wenger
 kocha wa Arsenal

 Hapa kulikuwa na mpambano 
mkali sana kati ya Peter Crouch 
wa Stoke na walinzi wa Arsenal



Manchester United Dhidi ya Fulham 
 Man United walinda magoli 3-2 dhidi ya Fulham. Ikumbukwe kuwa mechi yao ya kwanza walifungwa na Everton 1-0.

 Huyu hapa juu ni Usain Bolt, 
mfukuza upepo maarufu sana, 
raia wa Jamaica ambaye ametokea 
kuwa mshabiki mkubwa wa 
Manchester United. Hapa alikuwa katikati ya
 uwanja kabla ya kuanza kwa mechi
 ya Man United dhidi ya Fulham.

 Wayne Rooney akipelekwa nje baada 
ya kujeruhiwa vibaya sana kwenye paja lake. 
Inasemekana atakaa nje  ya dimba kwa 
wiki nne mfululizo akiuguza jeraha.

 Usain Bolt na ushabika wake kwa Man United.

 Wayne Rooney akichati na Welbeck kabla hawajaingia uwanjani 


 Robin Van Persie akifunga goli la kusawazisha 
kwa Man United kwa ufundi wa hali ya 
juu kama ilivyo kawaida yake. 
Na hili ndilo goli lake la kwanza tangu 
ajiunge na Man United.

 Shinji Kagawa akishangilia baada ya
 kufunga goli la pili kwa Man United

 Rafael Da Silva akishangilia baada ya 
kufunga goli la tatu kwa Man United

 Juu na chini, hapa ndiyo wakati 
Wayne Rooney anaumia

Chelsea Dhidi Ya Newcastle
Chelsea waliwafunga Newcastle magoli 2-0

 Juu: Eden Hazard


 Torres akishangilia goli






No comments:

Post a Comment