Wednesday, 29 August 2012

Huyu Hapa Ni Usain Bolt

Usain Bolt amejizolea sifa kubwa 
sana duniani baada ya kuonesha 
umwamba wake wa mbio za mita 
100 na 200 kwenye michezo ya 
Olympic iliyofanyika mwezi uliopita
 huko London Uingereza.


 Mara zote alikuwa anatamba kwamba 
atashinda  kabla ya mbio kufanyika 
na wakati wa mbio ndicho alichofanya
 na kusababisha watu wengi wa
 mataifa mbalimbali kuvutiwa 
naye na kumpenda sana.


 Ilifikia hata watu wa mataifa mengine 
walimshangilia kwa nguvu zote



Imegundulika kwamba Usain Bolt 
ni mshabiki mkubwa sana wa 
Man United na anapokuwa 
England hujaribu kuhudhuria 
mechi zote za Mashetani hao wekundu.


Kuna wakati alisikika akisema 
kwamba anamwomba Sir Alex Ferguson 
amsajili kwenye kikosi chake 
kwani pamoja na kuwa na wachezaji 
wenye vipaji pia timu inahitaji 
wachezaji wenye mbio kama yeye.

No comments:

Post a Comment