Wednesday, 22 August 2012

Chelsea 4, Reading 2


Hivi ndivyo ilivyokuwa kwenye mechi ya 
English Premier League jana Jumatano kati ya Chelsea 
na Reading huko Stamford Bridge ambapo Chelsea 
waliibuka na ushindi wa magoli 4-2.

Frank Lampard akifunga goli

Mchezo huo ulipigwa jana Jumatano ambapo 
kwa Reading iliyopanda daraja msimu huu ulikuwa 
ni wa kwanza kwake na kukaribishwa kwa kipigo hicho cha 4-2.

Reading wakishangilia baada ya Danny Guthrie
wa pili kushoto kufunga goli.

Hivi ndivyo Frank Lampard alivyofunga 
goli kwa penati kwenye dakika ya 18

Meneja wa Reading, Brian McDermott alilalamikia 
goli la Torres kwamba alikuwa offside wakati akifunga 
na hata alijaribu kumueleza mwamuzi msaidizi lakini 
haikusaidia kitu. Alisikika akisema kwamba ni kitendo 
cha aibu sana kwa refa kufanya kosa kama lile. 

Hivi ndivyo Danny Guthrie wa Reading alivyofunga goli.

Wakati chelsea walipopata goli la penati kwa shuti la
 Lampard, Reading walikuja juu kupitia Pavel Pogrebnyak 
alipofunga goli la kwanza kwa kichwa na 
Danny Guthrie kufunga la pili kwa shuti la moja kwa moja.

Branislav Ivanovic wa Chelsea akifunga goli la nne

Katika dakika ya 69 Gary Cahill naye alipiga 
shuti la mbali lilimfanya kipa wa Reading 
Adam Federici ausindikize mpira nyavuni.

Ndivyo lilivyokuwa goli la Torres

Kwa mtindo huu inaonesha Chelsea wamedhamiria sio tu kuwa mabingwa wa Ulaya bali hata kulitwaa kombe la English Premier League linalowaniwa kwa nguvu zote na Man United ambao walinyang'anywa msimu uliopita na mahasimu wao Man City ambapo Man City nao wanataka kulibakiza kwani mechi yao ya kwanza pia waliianza vizuri japo walishinda kwa mbinde sana.

Msomaji unaweza ukatabiri ni nani atakuwa bingwa wa Uingereza mwaka huu? Kazi kwako..!!

No comments:

Post a Comment